TANGAZA NASI KWA BEI NAFUU

Jumanne, 14 Mei 2013

WANAFUNZI WA SHULE YA SEKONDARI MANZESE WAVAMIWA NA MASHETANI NA KUANGUKA HOVYO


https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgdg0rznxiSSqBYnsBd8VHA0Em6Jw2LpPXp3O_H_EqZjR1ObDf-sULiSk0ivRCOScoQF73tnK9ZYWVTkqIdw7gPiMFO7YyK7Y75enWlb3MqKBeCGa38WnRL4WtGKzHCNR-r51KiNh3R3Dt_/s1600/maz.jpg
Mmoja kati ya wanafunzi wa shule ya Sekondari Manzese, ambaye hakuweza kufahamika jina lake mara moja aliyeanguka na kuweweseka leo mchana wakati akiwa shuleni hapo jambo ambalo lilizua hofu kubwa kwa wazazi na wanafunzi wa shule hiyo, huku baadhi ya wanafunzi wakitimua mbio huku na
 huko bila kujitambua, jambo lililomfanya Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo kuwarusu wanafunzi wote kurejea majumbani na kukatis masomo. Haikuweza kufahamika mara moja chanzo cha tatizo hilo, huku Maustaadh na wachungaji wakifika shuleni hapo na kuwaombea waliopatwa na tatizo 
hilo na kukemea.
Imeelezwa kuwa wanafunzi wa shule hiyo iliyopo Manzese Uzuri, jijini 
Dar es Salaam, wamekumbwa na mashetani jambo lililowafanya kuwa wakianguka hovyo na kutimua mbio huku na huko madarasani huku 
wakipiga makelele na kuongea maneno yasiyoeleweka.
Mmoja wa Wachungaji waliowahi kufika shuleni hapo akimfanyia 
maombezi mmoja wa wanafunzi hao waliopatwa na tatizo hilo.
Hawa ni baadhi ya wanafunzi wakiwa hawajielewi.

Mmoja akikemewa ili kumtoa mashetani hayo baada ya kuanguka.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni